Wazee wafanya maombi ya kipekee katika makao ya Uhuru Kenyatta

July 2024 · 2 minute read

-Baraza la wazee Wakikiyu walifanya maombi maalum mara mbili

-Maombi hayo hasa ni ya kuitisha amani na kuchaguliwa tena kwa Rais Uhuru Kenyatta

-Hafla moja ya maombi ilifanywa nyumbani kwake Gatundu na nyingine ilifanyiwa msituni, Mlima Kenya Alhamisi

Baraza la wazee Wakikuyu lilifanya maombi maalum Agosti 3 kwa kujitayarishia uchaguzi mkuu wa Agosti 3.

Habari Nyingine: Mwanamke Mkenya akiri kushiriki ngono na wanaume 100, maisha yake yabadilika (picha)

Wazee hao walifanya maombi yanayofahamika kwa lugha ya Kikuyu kama Kiama Kia Ma.

Maombi hayo mara mbili yalifanywa Ichaweri, Gatundu Kusini, kuombea amani Agosti 8 na ushindi wa Rais Uhuru Kenyatta.

Pakua APP mpya ya TUKO upate habari BURE!

Siku hiyo, wazee katika Kaunti ya Nyeri pia walifanya maombi msituni, ndani ya Mlima Kenya, kuombea amani kabla na baada ya uchaguzi mkuu.

Kaunti ya Nyeri, kulingana na habari, ni ngome ya Uhuru Kenyatta. Kulingana na mzee mmoja Nyeri, Samuel Kagutha, maombi hayo yalifanywa katikati mwa msitu kwa sababu wanaamini kuwa nguvu za Mungu ni nyingi zaidi katikati mwa msitu huo.

Habari Nyingine: Picha za kufurahisha za Uhuru akiwa na watoto katika ziara zake za kampeni

Wazee hao walibeba vitu vya kutamaduni kama tango na bakuli ambazo zinaaminika kufukuza mapepo.

Pia, walitumia mwanakondoo. Kagutha alishutumu zaidi utengano wa kikabila nchini na kuongeza kuwa hiyo ilikuwa kazi ya wakoloni.

“Kenya sio nchi ya ukabila, utengano tunaoshuhudia uliletwa na wakoloni,” alisema Kagutha.

Subscribe to watch new videos

Subscribe to Tuko youtube channel to watch more interesting videos

Read ENGLISH VERSION

Una maoni?Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiaYV2hJRmrpqylZp6uK3FmqWymV2irrC5waJkspldoLaxscqenGajkam2rK2MppikmZ9ixqJ51KGsq61doLKvxcCtq5pmmKm6rQ%3D%3D