-Afisa mkuu mtendaji wa NASA Norman Magaya ameeleza kwamba viongozi wa NASA mipango ya kuunda serikali Januari 31
-Magaya aliwaahidi Wakenya kuwa serikali yao itaanza kazi moja kwa moja huku wakianza mipango ya kuunda serikali
Mkurugenzi mtendaji wa NASA Norman Magaya ameeleza kwamba serikali ya NASA imeanza mipango ya kuunda serikali Januari 31 huku wakiwatambua baadhi ya viongozi watakaoteuliwa kuwa mawaziri katika serikali hiyo.
Habari Nyingine:Kutana na mwanamke mrembo Mkorino anayewakosesha wanaume usingizi
Serikali ya NASA iliundwa punde tu baada ya kumwapisha Raila Odinga kama Rais wa wananchi Januari 30.

Norman Magaya sasa amejitokeza na kuwajibu Wakenya ambao walikuwa wakiuliza kuhusu kitakachofuata baada ya kumwapisha Raila Odinga kama rais.
Habari Nyingine:Hutoweza 'kutoboa' 2022 bila ya msaada wangu - Raila amwambia Ruto
‘’ Mazungumzo kuhusu uteuzi wa mawaziri unapaswa kuanza leo hii’’ Magaya alikiambia kituo cha redio Citizen.
Aidha, Magaya aliwaahidi wafuasi wa NASA kuwa atoa habari baadaye kuhusu mahali ambapo afisi za serikali hiyo itawekwa.
Habari Nyingine:Manchester United yaorodheshwa kuwa klabu tajiri kote ulimwenguni
Awali, Jarida la TUKO.co.ke liliripoti kuhusu jinsi waziri Matiangi alivyoeleza kwamba uchunguzi umeanza kuhusiana na uapisho haramu uliofanywa na muungano wa NASA Januari 30 katika bustani ya Uhuru.
Read ENGLISH VERSION
Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe? Tuma ujumbe kwa mhariri: mwangi.muraguri@tuko.co.ke
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdia4F4g5Jmqp6qmaCurbWMsphmppGorm7FwJqls5ldoK67tYyrmKylmanCrLuMpJxmpJmjrm60wJuYq6FdoK6utcuiZaGsnaE%3D