- Itumbi Alhamisi Agosti 6 alisimulia kuhusu safari yake kazini katika Ikulu kuanzia 2013
- Alisema kuna kundi la watu ambao hawakutaka yeye na kikosi chake wachukue nyadhifa walizokuwa wamekabidhiwa na Rais Uhuru
- Mwanablogu huyo alisema ilibidi atumie ujanja ili wafaulu kujiunga na kikosi cha PPS alichokipa jina la PSCU baadaye
Aliyekuwa mwelekezi wa masuala ya kidijitali katika afisi ya rais Dennis Itumbi amesimulia safari yake kama mfanyikazi wa Ikulu kuanzia 2013 na aliyoyapitia.
Itumbi alisema haikuwa rahisi kwake na wenzake kuajiriwa na Ikulu kwani kuna watu walitaka watupwe nje baada ya Rais Uhuru Kenyatta na William Ruto kushinda urais 2013.
Habari Nyingine: Mgeni wa DP Ruto apatikana na coronavirus siku mbili baada ya kutembea Karen

Alisema ahadi ilikuwa wote walioteuliwa kama kikosi kipya kwenye kitengo cha habari cha rais watangazwe wakati Rais aliita mkutano Ikulu na wahariri kutoka vyombo mbali mbali lakini hilo halikufanyika.
"Usiku kuna mtu alibadilisha hotuba ya rais na kuondoa majina yetu akiache tu lile la Manoah (aliyeteuliwa msemaji wa Ikulu).
Tuliketi hapo tukisubiri kikosi chetu kizinduliwe lakini hilo halikufanyioka," alisema Itumbi.
Habari Nyingine: Kura ya maoni: Uhuru ameshindwa kutatua mzozo wa bunge la kaunti ya Nairobi

Itumbi alisema ilimlazimu kutumia ujanja ili kukubaliwa kuchukua nafasi ambazo walikuwa wameteuliwa kuchukua.
"Niliomba Mwenyezi Mungu na kuanza mikakati. Nikaandika taarifa kwa vyombo vya habari na kuita kikosi hicho Presidential Strategic Communication Unit," alisema Itumbi.
Baada ya hapo Itumbi alimtafuta Rais na kumtaka atie sahihi taarifa hiyo ili itumwe kwa vyombo vya habari.
Habari Nyingine: Zubeidah Koome: Mtangazaji aonyesha miradi yake ya kutafuta pesa zaidi

Kulingana na mwanablogu huyo, ni hatua yake ya kutoa taarifa hiyo ambapo waliweza kufaulu kuchukua nafasi walizoahidiwa.
"Kwa mwaka mzima tulifanya kazi bila mshahara na tuliruhusiwa kuingia Ikulu kwa sababu tu ya taarifa niliyotumwa kwa vyombo vya habari," aliongeza.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjbH91gphmq66kmZuur8XAZqKasplitqzBy65kpq%2BRoK5uudmipJplkp65onnKrqOiqKeWeqWxzaegrGWZqcKurshmmKydnZZ7qcDMpQ%3D%3D